Kile ambacho unawaambia watu wakipitia ndio unapaswa kujiambia pia ukipitia hali hiyo, mfano mtu amepatwa na ugonjwa kuna maneno unamuambia ya kumpa pole nawe ukiumwa unapaswa kujiambia maneno hayo kwanza ili kujikumbusha kuna watu pia wamewahi kupitia hali hiyo, kama mtu akipata na msiba kuna maneno ya Pole ambayo tunayatoa ya faraja ambayo mengine yanatokana na imani zetu nayo pia tunapaswa kujiambia tukiwa tunapitia hali hizo hii inatusaidia kujipa moyo na kutokata tamaa pale tunapopitia hali hizo.
Tafakari ya kufikirisha 80/366-2024
by
Tags:
Leave a Reply