Kwa kila ushauri unaoupata kutoka kwa wengine, usikimbilie tu kuufanyia kazi, hata kama ushauri huo umekuwa na manufaa kwao.
Unapaswa kujitathmini kwanza hatua uliyopo sasa na kule unakotaka kufika. Kisha jiulize kama ushauri unaopewa ni wa jumla au maalumu kwako.Kuna wakati mtu unaweza kufanyia kazi ushauri unaopata na ukazidi kurudi nyuma badala ya kwenda mbele.
Hiyo inatokana na kutumia ushauri wa jumla wakati ulihitaji ushauri maalumu kwenye jambo lako Nukuu Toka kwa Dr. Makirita Amani.
Tafakari ya kufikirisha 17/366-2024
by
Tags:
Leave a Reply