Njia pekee ya wewe kuwa na furaha kwenye maisha, ni kujua vitu gani unajali, kisha kuvifanya kwa ubora wa hali ya juu sana.Kila mmoja wetu kina vitu ambavyo anavijali zaidi kwenye maisha. Kwa wengine inaweza kuwa kazi au biashara, wengine mahusiano yao, wengine eneo fulani la kazi, wengine kuwasaidia watu, wengine kuishi kulingana na falsafa au dini wanayoamini. Maswali ya kujiuliza Je vitu gani ninavyojali sana kwenye maisha yangu?Vitu gani nipo tayari kufanya hata kama hakuna anayeangalia au anayenilipa?Je kazi au biashara ninayofanya, inahusisha vile vitu ambavyo ni muhimu zaidi kwangu, vile ? Je ni kitu gani kinakupa furaha zaidi kwenye maisha yako? Tenga dakika 5 mpaka 10 kujiuliza maswali hayo kila siku na ujipe majibu sahihi Nukuu toka kwa CICERO
Tafakari ya kufikirisha
by
Tags:
Leave a Reply